
JAJI Eliezer Feleshi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), amesema yupo pamoja na wanahabari katika safari ya mabadiliko ya sheria zinazohusu tasnia ya habari nchini.
Ametoa kauli hiyo leo tarehe 13 Juni 2022, ofisini kwake bungeni, jijini Dodoma alipokutana na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) na wadau wengine wa habari.
Amesema, katika mabadiliko ya haraka, kuna mambo mengi yaliyotokea na makovu yake hayawezi kufutika kwa haraka.
“Sishangai yote yaliyotokea hapa katikati katika kipindi cha transformation (mabadiliko), katika mabadiliko ya haraka, makovu huwa hayafutiki haraka,” amesema Jaji Feleshi.

Miongoni mwa kasoro hizo ni pamoja na mwanahabari kuweza kufungwa bila hata kuitwa mahakanai kujitetea, kuundwa vyombo vingi vitakavyoelemea wanahabari, dhana kutumika kufunga wanahabari lakini pia vyombo vya habari kufungwa bila kufikishwa mahakamani.
James Marenga, Makamu Mwenyekiti wa MISA- TAN, amemweleza Jaji Feleshi kuwa, wadau wa habari wanashirikiana ili kufika malengo ya mabadiliko ya sheria zinazominya uhuru wa habari nchini.
Be the first to comment